Bao la dakika ya 45 kipindi cha kwanza kupitia mpira wa adhabu kutoka kwa Jean Charles Houa limetosha kuipa Simba ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya Stellenbosch katika mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya kombe la Shirikisho (CAC CC)
Ulikuwa mchezo wa vipindi viwili, Simba ilitawala na kutengeneza nafasi nyingi katika kipindi cha kwanza huku Stellenbosch wakicheza kwa kujihami zaidi na kutumia mashambulizi ya kushitukiza
Kipindi cha pili mkufunzi wa Simba Fadlu Davids alibadili mbinu akiwaacha Stellebosch kumiliki mchezo huku Simba ikitumia mashambulizi ya kujibu
Kulikuwa na nafasi ya Simba kumaliza mchezo dakika za majeruhi lakini Ahoua alishindwa kutumia nafasi adimu ambayo ni wazi ingeweza kuifanya Simba iende Afrika Kusini kwenye mchezo wa pili ikiwa na ushindi mnono zaidi
Pengine mashabiki walitamani ushindi wa mabao mengi lakini hii ni nusu fainali na katika hatua hii hakuna timu dhaifu
Simba itakuwa katika nafasi nzuri ya kusonga mbele hatua ya fainali endapo itashinda mchezo wa marudiano au sare yoyote na zaidi itakuwa na faida kubwa kama itafunga bao la ugenini



