Mshambuliaji wa Yanga Clement Mzize anaongoza mbio za kuwania tuzo ya ufungaji bora msimu huu 2024/25
Mabao mawili aliyofunga katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Fountan Gate na kuihakikishia Yanga ushindi wa mabao 4-0, yamemfanya afikishe mabao 13 na kuwapiku Prince Dube na Jean Ahoua waliokuwa wakiongoza mbio hizo na mabao 12
Msimu huu Mzize amevunja rekodi yake ya mabao tangu apandishwe kikosi cha kwanza kutoka Yanga B misimu mitatu iliyopita, akifunga zaidi ya mabao 10
Msimu uliopita alifunga mabao sita na kutoa asisti 7. Je ataweza kubakia kileleni hadi mwisho wa msimu na kubeba kiatu cha dhahabu?




