Local,Normal News,Simba

Simba yabadilishiwa refa mechi dhidi ya Stellenbosch

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 Apr 2025
Simba yabadilishiwa refa mechi dhidi ya Stellenbosch

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limefanya mabadiliko ya refa wa mechi ya marudiano ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baina ya Stellenbosch na Simba itakayochezwa Jumapili, Aprili 27, 2025.

Awali refa aliyepangwa kuchezesha mechi hiyo alikuwa ni Amin Omar kutoka Misri na sasa timu hizo zitachezeshwa na Mohamed Maarouf Eid Mansour ambaye naye anatoka Misri.

Haijafahamika bado sababu za CAF kuchukua uamuzi huo wa kumbadilisha Amin Omar ambaye hana historia nzuri na Simba katika mashindano ya kimataifa.

Kumekuwa na usiri mkubwa katika ufanyaji wa mabadiliko hayo na utangazwaji wake na CAF kuelekea mchezo huo uliobeba hisia na mvuto mkubwa kwa nchi za Afrika Kusini, Tanzania na Afrika kiujumla.

Mwamuzi Mansour atasaidiwa na wenzake kutoka Misri ambao ni Mahmoud Abouelregal na Ahmed Ibrahim ambao ilikuwa tangu awali wawe wasaidizi lakini pia kuna mabadiliko kwa refa wa akiba ambapo sasa atakuwa Mahmoud Nagy naye kutoka Misri.

Mtathmini wa marefa ni Bechir Hassani kutona Tunisia na Kamishina wa mechi ni Kelesitse Gilika wa Botswana.

Hakuna mabadiliko upande wa marefa wanaosimamia teknolojia ya video ya usimamizi kwa marefa (VAR) ambapo kuna Mahmoud Ashour na Mahmoud Elbana wote kutoka Misri.

Simba imewahi kukutana na refa Mansour mara mbili ambapo ya kwanza alikuwa refa wa kati ilipotoka sare ya bao 1-1 nyumbani na Asec Mimosas kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2023/2024 na mechi ya pili alikuwa refa wa akiba ilipoibuka na ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Horoya msimu huohuo

Mwanaspoti

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
3h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
7h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
9h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
10h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
10h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’