Ndio! kazi imemalizika dimba la Moses Mabhida Simba ikirejea kile ilichofanya mwaka 1993 ikitinga fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho baada ya suluhu ya bila kufungana dhidi ya Stellenbosch
Ulikuwa mchezo ambao Simba iliingia kimkakat zaidi ikihitaji ushindi au matokeo ya sare kufuatia ushindi wa ao 1-0 ambao waliupata katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa visiwani Zanzibar
Haikuwa kazi rahisi lakini kocha Fadlu Davids aliandaa mpango mkakati na wachezaji wakaweka nguvu zao zote na nidhamu ya hali ya juu kuhakikisha lengo la kutinga fainali linafanikiwa
Ama kwa hakika msimu huu ni wa kipekee kwa Simba, uwekezaji wa Bilionea Mohammed Dewji na kile alichokuwa akitamani kuleta taji la CAF Tanzania kinaonekana
Sasa Simba imebakisha dakika 180 tu kulileta kombe la Shiririkisho Tanzania
Mnyama anamsubiri mshindi wa mchezo kati ya CS Constantine dhidi ya RS Berkane na habari njema ni kuwa kwenye fainali Simba itaanzia ugenini na kumalizia nyumbani



