Local,Normal News,Simba

Baada ya kutinga fainali, Fadlu ataka ubingwa CAF CC

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Apr 2025
Baada ya kutinga fainali, Fadlu ataka ubingwa CAF CC

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amewapongeza wachezaji wake kwa kufanikiwa kutinga fainali ya kombe la Shirikisho (CAF CC) baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana dhidi ya Stellenbosch katika mchezo wa nusu fainali mkondo wa pili uliopigwa uwanja wa Moses Mabhida Jumapili jioni

Simba ilitinga fainali kwa ushindi wa jumla wa bao 1-0 kufuatia matokeo ya ushindi hao katika mchezo wa mkondo wa kwanza

Akizungumza baada ya mchezo huo, Fadlu alisema wachezaji wamethibitisha wanaweza kubadilika na kuhimili kila aina ya mchezo

"Katika mechi zilizopita tulionyesha tunaweza kutawala mchezo na kuwalazimisha wapinzani wetu kukaa nyuma lakini leo tumeonyesha tunaweza kucheza hata bila ya mpira"

"Wachezaji wangu wameonyesha wanaweza kupambana hata katika mechi ambazo tutalazimika kukaa nyuma kuzuia"

"Nawaongeza kwa kile walichofanya leo (jana), tuko karibu kufikia malengo yetu"

"Kwa sasa tunaweza kufurahi lakini kwa kiasi kwa sababu bado hatujamaliza kazi. Tuna mechi mbili za fainali, furaha kubwa tutaipata mwisho," alisema Fadlu

Hii ni mara ya pili Fadlu anaiongoza timu kucheza fainali ya kombe la Shirikisho akifanya hivyo msimu wa 2021/22 akiiongoza Orlando Pirates

Lakini pia kwa mara nyingine anakwenda kukutana na RS Berkane katika mchezo wa fainali ambapo fainali iliyopita May 22 2022 Pirates walipoteza kwa mikwaju ya penati baada ya matokeo ya sare ya bao 1-1

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
30m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’