Yanga mikononi mwa Zimamoto nusu fainali Ligi ya Muungano

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th April 2025


Yanga mikononi mwa Zimamoto nusu fainali Ligi ya Muungano

Jana kigogo mwingine kutoka Tanzania Bara Azam Fc aliaga michuano ya ligi ya Muungano akikubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa JKU katika mchezo wa nusu fainali

Kipigo hicho kimezfanya timu tatu kutoka Tanzania Bara Singida BS, Coastal Union na Azam Fc kuaga michuano hiyo inayofanyika Gombani, Pemba

Yanga ndio timu pekee iliyobaki kutoka Bara na leo itashuka dimba la Gombani kumenyana na Zimamoto katika mchezo wa pili wa nusu fainali utakaopigwa sa 1:15 usiku

JKU ambayo iliziondoa Singida BS na Azam Fc, tayari imetinga fainali ikisubiri mshindi wa mchezo wa leo kuelekea mechi fainali

Je Yanga itafanikiwa kwenda fainali leo au itaungana na wawakilishi wengine wa Bara kuaga michuano hiyo mapema?


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.