Kocha Msaidizi wa Simba Selemani Matola amesema timu iko tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mashujaa Fc ambao utapigwa kesho Ijumaa, May 02 katika uwanja wa KMC Complex
Akizungumza katika Mkutano na wanahabari mapema leo, Matola alisema wanatambua kila mchezo uliobaki kwenye ligi una umuhimu mkubwa katika kutimizamalengo ya msimu huu
Hivyo wanauchukulia mchezo huo kama fainali na dhamira iliyopo ni kuchukua alama zote tatu
Amesema wanatambua Mashujaa Fc sio timu nyepesi lakini wana imani kwenye ubora wa kikosi na hivyo matarajio ni kuchukua alama zote tatu
"Tumekuwa na maandalizi mazuri kuelekea mchezo huu. Tunauchukulia mchezo huu kama fainali kwani tunajua tunahitaji kushinda"
"Licha ya ubora wa Mashujaa Fc, lakini tunaamini tutakuwa bora zaidi yao na kwenda kupata alama tatu kama malengo yetu yalivyo," alisema Matola
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, kiungo Awesu Awesu amesema ari na morali kila mchezaji iko juu
Wanakwenda kucheza mechi hii kama walivyofanya katika mechi zilizopita na muhimu ni kuhakikisha alama zote tatu zinabaki Msimbazi
"Wachezaji wote tuko tayari, morali ya timu iko juu kuelekea mchezo huu. Tunauchukulia mchezo huu kwa uzito uleule kama mechi iliyopita"
"Namaini kwa maandalizi tuliyofanya, tutacheza vizuri na kuibuka na ushindi," alisema Awesu