International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi, May 1 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 May 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi, May 1 2025

Mshambuliaji wa Brazil Rodrygo, mwenye umri wa miaka 24, anafikiria kuondoka Real Madrid katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi baada ya kupoteza nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Bernabeu. (Radio Marca)

Manchester United na Juventus wanachuana kuwania saini ya kiungo wa kati wa Brazil, Ederson mwenye umri wa miaka 25 kutoka Atalanta. (Tuttosport)

Mshambuliaji wa England Harry Kane ameendelea kuhusishwa na kurejea Ligi Kuu England, lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 anapanga kusalia Bayern Munich kwa mwaka mmoja zaidi. (Talksport)

Mlinda mlango wa Aston Villa na Argentina Emiliano Martinez, mwenye miaka 32, pamoja na winga wa Jamaica Leon Bailey, 27, wanawindwa na vilabu vya Saudi Arabia. (Telegraph)

Bayern Munich wanaamini wako katika nafasi nzuri ya kumsajili kiungo mshambuliaji wa Ujerumani Florian Wirtz kutoka Bayer Leverkusen, ambaye anaweza kuuzwa kwa klabu nyingine iwapo atataka kuondoka. (Sky Sports Germany)

Kocha wa zamani wa Manchester United Erik ten Hag yuko kwenye orodha ya Bayer Leverkusen ya makocha wanaoweza kumrithi Xabi Alonso, ambaye anahusishwa na kuchukua nafasi ya Carlo Ancelotti huko Real Madrid. (Sky Sports Germany)

Kiungo mshambuliaji wa England Harvey Elliott, mwenye miaka 22, amekuwa na wakati mgumu kupata nafasi ya kucheza Liverpool msimu huu lakini anataka kubaki na kupambana kwa ajili ya nafasi yake. (Liverpool Echo)

Everton ni miongoni mwa vilabu vinavyomuwinda mshambuliaji wa Ipswich Town, Liam Delap mwenye miaka 22, ambaye anaaminiwa kuwa na kipengele cha kuuzwa kwa pauni milioni 30. Wakati huo huo, uwezekano wa mshambuliaji wa England Dominic Calvert-Lewin, 28, kusaini mkataba mpya na klabu hiyo haujatupiliwa mbali. (The i Paper)

Beki wa Korea Kusini Kim Min-jae anasema anatumai atasalia Bayern Munich, ingawa klabu hiyo inaonekana kuwa tayari kumuachia mchezaji huyo mwenye miaka 28 iwapo ofa nzuri itawasili. (Sport Bild)

Mshambuliaji wa Ufaransa Enzo Kana-Biyik, mwenye umri wa miaka 18, yuko mbioni kukamilisha uhamisho wake wa bure kwenda Manchester United kutoka Le Havre. (Manchester Evening News)

Kocha wa zamani wa Wolves na West Ham, Julen Lopetegui, amesaini mkataba wa kuwa kocha wa Qatar hadi Juni 2027. (Fabrizio Romano)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’