International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili May 04 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 May 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili May 04 2025

Mshambuliaji wa Ufaransa Christopher Nkunku, 27, ameamua kuondoka Chelsea msimu huu wa joto. (Sky Sports Ujerumani)

Beki wa Kiukreni Oleksandr Zinchenko, 28, huenda akaondoka Arsenal msimu huu wakati Borussia Dortmund ikionesha nia ya kumnyakua. (Football Insider)

Kiungo wa kati wa Marekani Weston McKennie, 26, amefikia makubaliano ya mdomo na Juventus kusalia katika klabu hiyo hadi 2028. (Fabrizio Romano)

Manchester United, Chelsea na Tottenham Hotspur ni miongoni mwa vilabu kadhaa vinavyotaka kumsajili beki wa kati wa Bournemouth Dean Huijsen, 20. (CaughtOffside)

Aston Villa watakuwa na shida kumnunua mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford, 27, kwa mkataba wa kudumu kutoka Manchester United ikiwa hawatafuzu Ligi ya Mabingwa. (Football Insider)

Maskauti kutoka Aston Villa walikuwa kwenye umati wa watu kumtazama mshambuliaji wa Uhispania na Porto Samu Aghehowa, 20, huku kukiwa na nia ya kumsajili msimu huu wa joto. (Record , externalvia Sports Witness)

Everton wanatafakari kuhusu kumrejesha mshambuliaji wa zamani Richarlison, 27, katika klabu hiyo, huku Tottenham Hotspur ikiripotiwa kuwa tayari kukubali ada ya pauni milioni 40. (GiveMeSport)

Real Madrid wanafikiria kumnunua mlinzi wa kulia wa Real Sociedad Jon Aramburu, 22. (Fichajes)

Leeds United wamemuongeza mshambuliaji wa AZ Troy Parrott, 23, kwenye orodha ya washambuliaji wao kufuatia kupandishwa kwao kwenye Ligi ya Premia. (TeamTalk)

Fiorentina wanakaribia kuongeza mkataba wa beki mwenye umri wa miaka 20 Pietro Comuzzo huku wapinzani wao wa Serie , Napoli wakimtaka. (Tuttomercato)

Liverpool wanaweza kufanya uhamisho wa mshambuliaji wa Real Madrid Rodrygo, 24, huku Mbrazil huyo akiwa tayari kuhama Uhispania. (GiveMeSport)

Ajax wako tayari kumuuza mlinzi wa Uholanzi Jorrel Hato, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 akivutiwa na vilabu kama Chelsea. (Kick-off podcast)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’