Simba yalia ya ugumu wa ratiba NBC PL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th May 2025


Simba yalia ya ugumu wa ratiba NBC PL

Kocha Msaidizi wa Simba Selemani Matola amesema wamejipanga kuibuka na ushindi katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya KMC ambao utapigwa leo Jumapili katika uwanja wa KMC Complex licha ya ratiba ngumu inayowakabili

Akizungumza katika Mkutano na wanahabari jana, Matola alisema wamekosa muda wa kutosha wa maandalizi ya mechi kutokana na ratiba inayowalazimu kucheza kila baada ya siku tatu

Matola amesema wanajivunia kuwa na kikosi kipana kwani licha ya mabadiliko wanayofanya katika kila mechi, wameendelea kuibuka na ushindi

"Ratiba yetu ni ngumu kwani hatupati muda wa kutosha wa maandalizi lakini tuna kikosi kipana ambacho kinatuwezesha kupata ushindi popote"

"Tunafahamu mchezo dhidi ya KMC utakuwa mgumu lakini sisi tumejipanga kuhakikisha tunapata matokeo chanya," alisema Matola

Simba leo inacheza mechi ya nne katika kipindi cha siku 10 ikishinda mechi tatu zilizopita dhidi ya Mashujaa Fc (2-1), JKT Tanzania (1-0) na Pamba Jiji (5-1)

Baada ya mchezo dhidi ya KMC, Simba itasafiri Morocco kumenyana na RS Berkane katika mchezo wa mkondo wa kwanza fainali ya kombe la Shirikisho (CAF CC) utakaopigwa May 17


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.