Local,Normal News,Yanga, Namungo

Kocha Yanga anazitaka alama tatu dhidi ya Namungo Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 May 2025
Kocha Yanga anazitaka alama tatu dhidi ya Namungo Fc

Kocha Mkuu wa Yanga Miloud Hamdi amesema wamepata muda wa kutosha kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc ambao utapigwa kesho Jumanne katika uwanja wa KMC Complex

Akizungumza katika mkutano na wanahabari mapema leo, Hamdi alisema umepita muda mrefu hawajacheza mechi ya ligi kuu hivyo malengo ni kuendeleza pale walipoishia

Hamdi amesema anafahamu Namungo Fc wanahitaji angalau alama moja kutoka mechi zilizobaki ili kujihakikishia kuendelea kucheza ligi kuu msimu ujao

Hivyo anajua wataingi katika mchezo huo wakiwa na lengo la kupata angalau droo lakini kwa Yanga huo ni mchezo ambao lazima washinde

"Nafurahi tumepata muda mrefu wa kujiandaa na mchezo huo. Mechi zilizopita tulicheza kila baada ya siku tatu lakini ukiangalia mara ya mwisho tulicheza mechi ya ligi kuu April 21"

"Hii ni mechi ambayo upande wetu ushindi ni matokeo ya lazima ili kuhakikisha tunaendelea kusalia kileleni katika msimamo wa ligi"

"Nafahamu Namungo Fc wanahitaji angalau alama moja tu ili kujihakikishia nafasi ya kubaki ligi kuu msimu ujao, hivyo sare yatakuwa matokeo mazuri kwao"

"Hatuna nafasi ya kufanya makosa katika mchezo huu, tunachohitaji ni ushindi, tofauti ya alama moja katika msimamo huku zikisalia mechi tatu inatulazimu kushinda kila mchezo ili kuweza kutimiza malengo yetu," alisema Hamdi

Akizungumzia hali ya kikosi, Hamdi amesema baadhi ya wachezaji waliokuwa majeruhi kama Chadrack Boka, Khalid Aucho na Pacome Zouzoua wamerejea mazoezini na wenzao lakini hatma ya kutumika katika mchezo huo itategemea na utayari wao

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
48m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’