International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 13 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 May 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 13 2025

Manchester City inakusudia kumsajili kiungo Mholanzi Tijjani Reijnders (26) kutoka AC Milan, ambao watamuuza kama ofa ya zaidi ya pauni milioni 57 itatolewa (Telegraph)

Uongozi wa Manchester United hauna mpango wa haraka wa kumfukuza kocha wao Ruben Amorim (Talksport)

Winga wa Colombia Luis Diaz (28) ameahidi kusalia Liverpool licha ya kuhusishwa awali na Barcelona. (Express)

Real Madrid bado haijatoa ofa rasmi kwa Liverpool kumsajili beki wa kulia Trent Alexander-Arnold (26), ingawa walimuulizia wiki iliyopita kwa ajili ya Kombe la Dunia la Klabu mwezi ujao. (Sky Sports)

Liverpool inaweza kumchukua Jeremie Frimpong (24) wa Bayer Leverkusen na mholanzi, ambaye ana kipengele cha kuuzwa kwa pauni milioni 29.4-33.6. (Sky Germany)

Beki wa Newcastle Sven Botman (25) anataka kubaki kwenye klabu hiyo licha ya kuvutiwa na Paris St-Germain. (The I)

Napoli wamefanya mazungumzo na upande wa Kevin de Bruyne kuhusu uwezekano wa kumsajili bure msimu wa joto atakapomaliza mkataba na Manchester City. (Sky Switzerland)

Atletico Madrid wanapanga kufanya mazungumzo na Manchester United kuhusu usajili wa winga wa Brazil Antony (25), ambaye kwa sasa yupo kwa mkopo Real Betis, huku Juventus na Villarreal pia wakimhitaji. (Football Espana)

Real Madrid wanavutiwa na mpango wa kumrejesha beki wa kushoto wa Ufaransa Theo Hernandez (27) kutoka AC Milan, miaka sita baada ya kuondoka klabuni hapo. (Calciomercato)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’