Local,Normal News,Simba, Berkane

Fadlu apania kuiduwaza RS Berkane, Morocco

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 May 2025
Fadlu apania kuiduwaza RS Berkane, Morocco

Mkufunzi wa Simba Fadlu Davids amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa mkondo wa kwanza fainali ya kombe la Shirikisho (CAF CC) dhidi ya RS Berkane ambao utapigwa Jumamosi, May 17 katika uwanja wa Manispaa ya Berkane

Akizungumza katika Mkutano wa mechi hiyo, Fadlu amesema licha ya kikosi chake kusheheni vijana wengi wadogo ambao hawana uzoefu mkubwa na michuano hiyo, wamejipanga kukabiliana na Berkane na lengo ni kupata matokeo mazuri katika mchezo huo

"Nawafahamu RS Berkane, tulicheza nao misimu michache nyuma wakati nikiwa na klabu ya Orlando Pirates. Ni timu yenye uzoefu mkubwa na michuano hii"

"Licha ya timu yangu kuwa na vijana wengi wadogo, tumejipanga kuhakikisha tunafanya vizuri katika mchezo huu," alisema Fadlu

Kocha huyo raia wa Afrika Kusini aliongeza kuwa wanafahamu wanakwenda kucheza mechi ya kwanza ya fainali hapo kesho na wiki ijayo kutakuwa na mechi ya pili ambayo Simba pia itakuwa na nafasi ya kutumia uwanja wa nyumbani

Kocha Fadlu ameeleza kuridhishwa na sehemu ya kuchezea (pitch) ya uwanja wa Manispaa ya Berkane na kuongeza kuwa watakuwa tayari kupeperusha vyema bendera ya Simba katika uwanja huo

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, beki Che Malone Fondoh amesema katika hatua waliyofikia hawaihofii timu yoyote na malengo yao ni kushinda mchezo huo

"Tumepata nafasi ya kucheza fainali, sisi kama wachezaji tunafahamu wajibu wetu, tunahitaji kushinda mchezo huu," alisema

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’