Leo Jumamosi, Mei 17, macho ya mashabiki wa soka barani Afrika yatakuwa yakielekezwa katika Uwanja wa Manispaa ya Berkane, Morocco, ambako klabu ya Simba SC ya Tanzania itachuana na RS Berkane ya Morocco kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza wa fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAF Confederation Cup). Mchezo huo utapigwa saa 4 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.



