Fadlu awatisha RS Berkane

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th May 2025


Fadlu awatisha RS Berkane

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema licha ya ubora wa RS Berkane wamejipanga kutumia vyema uwanja wa nyumbani na kushinda mchezo wa mkondo wa pili fainali ya kombe la Shirikisho ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar

Akizungumza katika mkutano na wanahabari kuelekea mchezo huo, Fadlu alisema dhamira ya Simba ni kuona wanatwaa taji la Shirikisho (CAF CC) na kuandika histori mpya katika soka la Tanzania

Aidha amesema mechi ya kwanza ambayo walipoteza kwa mabao 2-0 nchini Morocco ilikuwa kama somo kwao hivyo wanafahamu namna ya kucheza mechi hiyo ya pili

"Tunafahamu Berkane ni timu ya daraja la juu barani Afrika kwa sasa lakini hawakukutana na Simba iliyo kwenye ubora na uwezo wake kamili"

"Tuko tayari kukabiliana nao na niseme tu, watakutana na hasira ya Simba. Mechi ya kwanza tumeitumia kama somo kuelekea mchezo huu wa pili," alisema Fadlu

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, nahodha msaidizi wa Simba Shomari Kapombe alisema walitamani mchezo huo upigwe katika uwanja wa Benjamin Mkapa lakini sasa kile ambacho walipanga kukifanya dimba la Mkapa, watakifanya hapo New Amaan Complex

"Tunafahamu kila mchezaji, Mwanachama na shabiki wa Simba alitamani mchezo huu upigwe uwanja wa Benjamin Mkapa lakini gatuwezi kupinga kilichoamuliwa na Mamlaka"

"Kile tulichopanga kukifanya uwanja wa Benjamin Mkapa, tutakifanya hapa uwanja wa New Amaan Complex," alisema Kapombe


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.