Local,Transfer News,Yanga

Chama njia panda Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 May 2025
Chama njia panda Yanga

Wakati msimu wa ligi kuu ukitarajiwa kufika tamati mwezi ujao, tayari michakato ya usajili inaendelea kwa nyota ambayo mikataba yao inaelekea ukingoni

Taarifa kutoka Yanga ni kuwa klabu hiyo ilianza mapema michakato ya kuhuisha mikataba ya wachezaji wake ambayo inamalizika mwishoni mwa msimu

Mpaka sasa wachezaji kama Pacome Zouzoua, Maxi Nzengeli, Dickson Job tayari wameramba mikataba mipya huku wachezaji wengine kama Khalid Aucho na Clatous Chama mazungumzo yakiwa yanaendelea

Hata hivyo kwa upande wa Chama imeelezwa kiungo huyo wa zamani wa Simba amepewa ya mkataba wa mwaka mmoja ambao thamani yake imezingatia mchango wake katika kikosi cha Yanga msimu huu

Kuna taarifa pia waajiri wake wa zamani Simba wanapambana kutaka kumrejesha kiungo huyo aliyejijengea heshima kubwa katika soka la Tanzania

Katika msimu wake wa kwanza na Yanga, Chama amekuwa na wakati mgumu kupenya katika kikosi cha kwanza mbele ya Stephane Aziz Ki na Pacome Zouzoua ambao wamekuwa katika ubora mkubwa

Chama amefunga mabao manne na kutoa asisti mbili katika ligi kuu ya NBC ambazo zaidi ya asilimia 80 ya mechi alizocheza, alitokea bench

Hata hivyo baada ya Aziz Ki kuondoka, pengine ni nafasi yake kurejea katika kikosi cha kwanza lakini pia msimu ujao eneo analocheza linatarajiwa kuwa na ushindani zaidi kwani Yanga inatarajiwa kusajili kiungo mwingine kuchukua nafasi ya Aziz Ki

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
44m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’