Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 27 2025

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th May 2025


Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 27 2025

Manchester City wanaharakisha harakati zao za kumsajili kiungo wa AC Milan na Uholanzi, Tijjani Reijnders, 26, ambaye anatarajiwa kugharimu zaidi ya pauni milioni 55. (Mail)

Kiungo wa Brazil, Casemiro, 33, na winga wa Argentina, Alejandro Garnacho, 20, ni miongoni mwa wachezaji ambao Manchester United wanataka kuwaondoa wakati huu wakipunguza kikosi chao kwa kiasi kikubwa kwa ajili msimu ujao. (Telegraph)

Manchester United wamefanya mazungumzo na mshambuliaji wa Brentford na Cameroon, Bryan Mbeumo, 25, ambaye anathamani ya takribani pauni milioni 50. (Talksport)

Newcastle United wanafanya mazungumzo magumu na mshambuliaji wa England Under-21, Liam Delap, 22, wanapojaribu kumshawishi mchezaji huyo wa Ipswich Town kujiunga nao badala ya kwenda Everton, Manchester United au Chelsea. (TeamTalk)

Newcastle pia wana nia kubwa ya kumsajili mshambuliaji wa Brazil wa Brighton, Joao Pedro, 23. (i Paper)

Chelsea wanaangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa wa Eintracht Frankfurt, Hugo Ekitike, 22. Pia wana nia kubwa ya kumsajili mshambuliaji Msweden wa Sporting, Viktor Gyokeres, 26, na Delap wa Ipswich. (Independent)

Eintracht Frankfurt wameweka dau la Ekitike, anayetakiwa na Chelsea, la pauni milioni 84, ingawa kwa muundo wa malipo unaoweza kujadiliwa. (Athletic)

Kiungo wa Uingereza na Sunderland, Jobe Bellingham, 19, yuko Ujerumani kwa mazungumzo ya kuhamia Eintracht Frankfurt, siku mbili baada ya kuisaidia klabu yake kupanda daraja. Borussia Dortmund, ambapo kaka yake Jude alicheza na Leipzig pia wanavutiwa naye. (Sky Sports)

Manchester United wanamtaka beki wa kulia wa Wolves na Ureno, Nelson Semedo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 atakuwa huru msimu huu wa joto. (Football Transfers)

Mkurugenzi wa michezo wa Bayer Leverkusen, Simon Rolfes, amethibitisha nia ya Liverpool kutaka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 22, Florian Wirtz. (Sky Sport Germany)

Mkurugenzi wa michezo wa Napoli, Giovanni Manna, anasema wamekuwa wakifanya kazi kwenye makubaliano ya kumsajili kiungo wa Ubelgiji Kevin de Bruyne, 33, kwa muda mrefu na "wanaweza kumpata sasa". Mkataba wake Manchester City unaisha mwezi ujao. (Rai News)

Chelsea, Bayern Munich na Manchester United zote zimeonyesha nia thabiti ya kumsajili mshambuliaji wa AC Milan na Ureno, Rafael Leao, 25, msimu huu wa joto. (Teamtalk)

Newcastle wameamua kutotumia fursa ya kumuongezea mkataba mshambuliaji wao wa zamani wa England mwenye umri wa miaka 33, Callum Wilson. (Athletic)

Wageni wapya wa Ligue 1, Paris FC, wanavutiwa kumsajili kiungo wa Senegal mwenye umri wa miaka 35, Idrissa Gueye, ambaye mkataba wake Everton unaisha mwezi ujao. (Foot Mercato)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.