Simba yapania ushindi dhidi ya Singida BS

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th May 2025


Simba yapania ushindi dhidi ya Singida BS

Kocha Msaidizi wa Simba Selemani Matola amesema wanahitaji kushinda mchezo wa ligi kuu dhidi ya Singida Black Stars hapo kesho ili kuhkikisha wanasalia katika mbio za ubingwa msimu huu

Akizungumza katika mkutano na wanahabari mapema leo, Matola alisema baada ya kikosi kurejea kutoka Zanzibar, moja kwa moja waliingia kambini kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya mchezo huo

Licha ya ugumu wa Singida Black Stars, Matola amesema ni matokeo ya ushindi pekee ambayo yatawabakisha katika mbio za ubingwa hivyo ni lazima washinde mchezo huo

"Sisi tuko tayari kwa mchezo huo, timu ilirejea salama kutoka Zanzibar na tunakamilisha maandalizi ya mchezo huu mgumu"

"Singida Black Stars ni moja ya timu ngumu msimu huu, ni timu imara ambayo ina wachezaji wengi wenye uzoefu mkubwa"

"Tulipokutana nao mara ya kwanza tulipata ushindi wa ao 1-0 ugenini lakini kila mmoja aliona jinsi mchezo ulivyokuwa mgumu"

"Lakini licha ya ugumu wao, kwetu sisi tunahitaji kushinda na tumejipanga kuondoka na alama zote tatu. Tunajua matokeo tofauti na ushindi yanaweza kuathiri malengo yetu ya kutwaa ubingwa msimu huu," alisema Matola

Simba na Singida Black Stars zitachuana katika mechi mbili zinazofuatana kwani baada ya mchezo wa ligi kuu, siku tatu baadae timu hizo zitachuana tena katika mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la CRDB ambao utapigwa uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara May 31


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.