International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Ijumaa May 30 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 May 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Ijumaa May 30 2025

Klabu ya Saudi Pro League, Al-Nassr, inamtaka Luis Diaz, 28, wa Liverpool, wakifuatilia hali ya mkataba wa winga huyo wa Colombia huko Anfield. (Telegraph)

Mabingwa wa Bundesliga, Bayern Munich, bado wana imani ya kumshawishi kiungo mshambuliaji wa Bayer Leverkusen, Florian Wirtz, 22, kujiunga nao msimu huu wa joto, na sio Liverpool. (SZ)

Chelsea wamevutiwa na kiwango cha Jadon Sancho hivi karibuni na wanaweza kutumia kipengele cha mkataba cha kumnunua kwa pauni milioni 25 walichokubaliana na Manchester United na kumsajili winga huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 25 kwa mkataba wa kudumu. (i Sport)

Brentford wako katika mazungumzo na Liverpool kuhusu mpango wa kumsajili kipa wa Jamhuri ya Ireland mwenye umri wa miaka 26, Caoimhin Kelleher. (Sky Germany)

Napoli wako karibu kukamilisha makubaliano ya masharti binafsi na mshambuliaji wa Canada mwenye umri wa miaka 25 wa Lille, Jonathan David, ambaye pia amewasiliana na Juventus. (Sky Sports)

Chelsea wamejiunga na Juventus kuzungumza na Sporting Lisbon kuhusu upatikanaji wa mshambuliaji wa Sweden mwenye umri wa miaka 26, Viktor Gyokeres, ambaye pia anasakwa na Arsenal. (Record)

Juventus wanavutiwa kumsajili mshambuliaji wa Brazil mwenye umri wa miaka 18 wa Real Madrid, Endrick, kwa mkopo. (Calciomercato)

Meneja wa zamani wa Juve, Massimiliano Allegri, anatarajiwa kurejea AC Milan kama meneja mpya. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 57 alitumia miaka minne San Siro kati ya 2010 na 2014. (Calciomercato)

Ipswich Town wamempa mshambuliaji wa Hispania mwenye umri wa miaka 19 wa Chelsea, Marc Guiu, mkataba wa mkopo ili acheze Championship msimu ujao. (Fabrizio Romano)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’