Fadlu, Mukwala washinda tuzo za ligi kuu Mei 2025

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th May 2025


Fadlu, Mukwala washinda tuzo za ligi kuu Mei 2025

Mshambuliaji wa Simba Steven Mukwala ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu kwa mwezi Mei 2025 akiwashinda Jean Charles Ahoua na Jaffar Kibaya wa Mashujaa Fc

Mukwala alicheza mechi nne katika mwezi Mei akifunga mabao matatu na kutoa pasi moja ya bao

AIdha tuzo ya kocha bora wa mwezi huo ilikwenda kwa kocha wa Simba Fadlu Davids aliyewashinda Rachid Toussi na Miloud Hamdi wa klabu za Azam Fc na Yanga

Fadlu aliiongoza Simba kushinda mechi zote tano mwezi Mei 2025


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.