Mshambuliaji wa Simba Steven Mukwala ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu kwa mwezi Mei 2025 akiwashinda Jean Charles Ahoua na Jaffar Kibaya wa Mashujaa Fc
Mukwala alicheza mechi nne katika mwezi Mei akifunga mabao matatu na kutoa pasi moja ya bao
AIdha tuzo ya kocha bora wa mwezi huo ilikwenda kwa kocha wa Simba Fadlu Davids aliyewashinda Rachid Toussi na Miloud Hamdi wa klabu za Azam Fc na Yanga
Fadlu aliiongoza Simba kushinda mechi zote tano mwezi Mei 2025




