Yanga itachuana na Singida Black Stars katika mchezo wa fainali ya kombe la Shirikisho la CRDB
Singida Black Stars imeifuata Yanga fainali leo baada ya kuifumua Simba mabao 3-1 katika mchezo wa nusu fainali uliopigwa uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara
Jonathan Sowah na Emmenuel Keyekeh ndio waliopeleka kilio Msimbazi wakifunga mabao muhimu kwa timu yao Keyekeh akifunga mabao mawili
Bao pekee la Simba katika mchezo huo lilifungwa na Jean Charles Ahoua kupitia mpira wa adhabu
Yanga ilikuwa ya kwanza kutinga fainali ikiichapa JKT Tanzania mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa May 18



