Yanga imeendelea kushikilia msimamo wake wa kutocheza mechi namba 184 ligi kuu ya NBC dhidi ya Simba hadi pale malalamiko yao yatakapofanyiwa kazi na mamlaka za soka nchini
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na mabingwa hao wa soka Tanzania Bara, mechi zilizobaki kuhitimisha msimu ni tatu tu
Juni 18 itacheza dhidi ya Tanzania Prisons (Ligi Kuu), Juni 22 dhidi ya Dodoma Jiji (Ligi Kuu) na mchezo wa mwisho ni fainali ya kombe la CRDB dhidi ya Singida Black Stars

Katika hatua nyingine, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amethibitisha kuwa timu hiyo imepokea mialiko ya kucheza mechi za kirafiki Rwanda na Kenya
"Ni kweli tuna mialiko miwili kutoka Rwanda na Kenya. Rayon Sports wametupa mwaliko kwenda kucheza nao mechi ya kirafiki lakini pia Gor Mahia wametualika Kenya"
"Uongozi unafanya tathmini na kutawataarifu mashabiki wetu wapi tunakwenda. Kama itakuwa Rwanda tutaandaa utaratibu wa safari kwa mashabiki pia"
"Hapo Rwanda tuna historia nafikiri wengi mnakumbuka tulichofanya miaka miwili iliyopita tulipokwenda kucheza na Al Merrikh," alisema Kamwe



