Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa vyanzo vya kuaminika, ni kwamba Ndugu George Mayawa, ambaye alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji wa Ligi maarufu kama Kamati ya Masaa 72, amejiuzulu
Kwa mujibu wa taarifa hizo, Mayawa amechukua hatua hiyo baada ya kutoridhishwa kwake na mwenendo wa sasa wa uendeshaji wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara.
Uamuzi huo umetajwa kuwa wa kimaadili na wenye lengo la kulinda hadhi ya mpira wa miguu nchini.
Mbali na nafasi hiyo, George Mayawa aliwahi pia kuhudumu katika Kamati ya Leseni za Klabu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), akiwa miongoni mwa wajumbe walioteuliwa katika awamu ya kwanza ya uongozi wa Rais Wallace Karia.
Hii ni hatua muhimu inayoashiria kuwepo kwa changamoto ndani ya mfumo wa uendeshaji wa ligi, na huenda ikawa chachu ya maboresho katika siku zijazo ingawa inaripotiwa kuwa kuna mengi ya kushangaza yanakuja siku za hivi karibuni.
Haya yanajiri wakati klabu ya Yanga ikishikilia msimamo wa kutocheza mechi dhidi ya Simba Juni 15 mpaka pale itakapopewa majibu kwa nini mchezo huo namba 184 haukufanyika March 08 tarehe iliyopangwa mwanzo
Yanga pia imeeleza kutokuwa na imani na baadhi ya viongozi wa Bodi ya Ligi ikiwataka Mtendaji Mkuu Almas Kasongo na Mwenyekiti Steven Mguto wawajibike



