Kikosi cha Simba kesho Alhamisi, Juni 05 kitaingia kambini kuanza maandalizi ya mechi tatu zilizobaki kuhitimisha msimu wa ligi kuu ya NBC 2024/25
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema wachezaji 9 ambao wameitwa timu za Taifa tayari wamejiunga na mataifa yao hivyo program za mazoezi zitawahusu wachezaji ambao hawana majukumu ya timu za Taifa
"Kikosi kinaingia kambini kesho Alhamisi kuanza maandalizi ya mechi tatu zilizobaki kuhitimisha msimu huu"
"Wachezaji ambao wameitwa katika timu za Taifa tayari wamejiunga na Mataifa yao hivyo Kocha Fadlu Davids na benchi lake la ufundi wataanza mazoezi na wachezaji waliobaki"
"Tunafahamu mchezo unaofuata ni dhidi ya Yanga, Juni 15 bado hatujataarifiwa mchezo huo utachezwa katika uwanjani gani lakini niseme tu maandalizi ya kuelekea mchezo huo tumeyaanza mapema," alisema Ahmed
Simba imebakisha mechi tatu dhidi ya Yanga (Juni 15), Kengold (Juni 18) na Kagera Sugar (Juni 22)



