Kikosi cha Simba kesho Alhamisi, Juni 05 kitaingia kambini kuanza maandalizi ya mechi tatu zilizobaki kuhitimisha msimu wa ligi kuu ya NBC 2024/25
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema wachezaji 9 ambao wameitwa timu za Taifa tayari wamejiunga na mataifa yao hivyo program za mazoezi zitawahusu wachezaji ambao hawana majukumu ya timu za Taifa



