Katika kipindi ambacho tetesi za usajili zinaendelea kushika kasi, jina la kiungo mahiri wa Azam FC, Feisal Salum ‘Fei Toto’, limekuwa likitajwa sana kuhusishwa na klabu ya Simba SC.
Hata hivyo, klabu hiyo kupitia kwa Meneja wa Habari na Mawasiliano, Ahmed Ali, imeweka mambo sawa – kwa sasa, ni kimya na heshima kwa mkataba wa mchezaji huyo.



