Bodi ya ligi (TPLB) wakati wowote inatarajiwa kutoa taarifa muhimu kuhusu mchezo wa ligi kuu namba 184 kati ya Yanga dhidi ya Simba ambao umepangwa kupigwa Jumapili, Juni 15 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Msemaji wa Bodi ya ligi Karim Boimanda amesema maandalizi ya msingi kuelekea mchezo huo yanaendelea vizuriΒ
"Maandalizi yako vizuri lakini pia ni vizuri nikitoa taarifa kwamba kuna baadhi ya taarifa nyeti na muhimu zitatolewa muda wowote kuanzia sasa"
"Taarifa hizo zinakwenda kuhitimisha mchakato mzima wa maandalizi kuelekea mchezo huo. Wadau wanapaswa kusubiri kusikia taarifa hizo kuhusiana na mchezo huo"
"Tunaendelea kusisitiza maandalizi ya mchezo yanaendelea tukiamini timu husika nazo zinaendelea na maandalizi pamoja na wadau wengine wa mchezo pia," alisema Boimanda
Simba imeweka msimamo wa kutokubali mabadiliko yoyote ya tarehe ya mchezo huo huku Yanga ikisisitiza haiko tayari kucheza Juni 15 pasipo matakwa yao kufanyiwa kazi