Uchaguzi Mkuu TFF kufanyika August 16 Tanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th June 2025


Uchaguzi Mkuu TFF kufanyika August 16 Tanga

Kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetangaza mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF utakaofanyika 16 August 2025 jijini Tanga

Katika uchaguzi huo nafasi zinazowaniwa ni Rais na Wajumbe 6 wa Kamati ya Utendaji

Gharama ya fomu ya Urais ni Tsh 500,000/- na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ni Tsh 200,000/-

Fomu zitaanza kutolewa Jumatatu Juni 16 hadi Juni 20 2025 Makao Makuu ya TFF na kwenye tovuti ya TFF


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.