International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu, Juni 16 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Jun 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu, Juni 16 2025

Real Madrid inatumai kumsajili beki wa Liverpool Ibrahima Konate, 26, kwa uhamisho wa bila malipo msimu ujao, mkataba wa Mfaransa huyo utakapokamilika. (Marca - kwa Kihispania)

Arsenal inataka sana kuwamsajili mshambuliaji wa Sporting na Uswidi Viktor Gyokeres, 27, na mshambuliaji wa RB Leipzig na Slovenia Benjamin Sesko, 22, Lakini ina uwezo wa kumsajili mshambuliaji mmoja tu msimu huu wa kiangazi. (Miror)

Hata hivyo, Arsenal inahisi gharama ya kumsajili Gyokeres iko juu mno hivyo huenda ikaamua kumsajili Sesko au mshambuliaji wa Aston Villa wa Uingereza Ollie Watkins, 29. (Record - kwa Kireno).

Timu hiyo ya Old Trafford imeamua kumbakisha mshambuliaji wa Uholanzi Joshua Zirkzee, 24. (Corriere dello Sport - kwa Kiitaliano)

Manchester United ilifanya mawasiliano na wawakilishi wa mshambuliaji wa Ufaransa Hugo Ekitike, 22, anayechezea Eintracht Frankfurt, wikendi hii. (Bild)

Klabu za EPL za Chelsea, Aston Villa na Tottenham zinaendelea kumfuatilia winga wa Manchester United Alejandro Garnacho, 20, baada ya Muargentina huyo kuambiwa yuko huru kuondoka. (Mail)

Klabu ya Al-Hilal ya Saudia imeboresha ofa yake kwa mshambuliaji wa Napoli na anayenyatiwa na Manchester United Victor Osimhen, 26, wakipendekeza mkataba na mshahara wa thamani ya hadi Β£42.6m kila mwaka. (Goal)

AC Milan imeanza mazungumzo na Arsenal kuhusu usajili wa beki wa The Gunners wa Ukraine Oleksandr Zinchenko, 28. (Corriere dello Sport - kwa Kiitaliano)

Klabu kadhaa za Ligi ya Premia na na Serie A zinamuulizia mshambuliaji wa Bayer Leverkusen wa Czech Patrik Schick, 29. (Sky Germany via Florian Plettenberg)

Paris St-Germain imefikia makubaliano ya kibinafsi na beki wa Bournemouth Illia Zabarnyi, 22, na imepiga hatua ada na klabu hiyo ya Ukraine. (Fabrizio Romano), nje

Galatasaray imewasilisha ombi la kumsajili mlinda lango wa Barcelona mwenye umri wa miaka 33 Marc-Andre ter Stegen. (Sport - kwa Kihispania)

Miamba ya Ureno Porto wanataka kumsajili winga wa Southampton Muingereza Tyler Dibling, 19. (Record - kwa Kireno)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’