Ili kuhakikisha hakuna upangaji wa matokeo ya namna yoyote, mechi za ligi kuu ya NBC raundi ya 29 na 30 zitapigwa saa 10 jioni
Mechi zote za raundi ya 29 zitapigwa leo Jumatano Juni 18 na raundi ya 30 zitapigwa Jumapili Juni 22 2025
Jumatano mabingwa watetezi Yanga watakuwa Mbeya kumenyana na Tanzania Prisons huku watani zao Simba wakiumana na KenGold mkoani Tabora
Wakati timu nyingine zitamaliza msimu Jumapili, Yanga na Simba zitahitimisha msimu siku ya Jumatano, Juni 25 dimba la Benjamin Mkapa kwa mchezo namba 184 kupigwa



