Mshambuliaji wa Yanga Prince Dube huenda akakosa mechi zilizosalia kuhitimisha msimu baada ya kupata majeraha katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons uliopigwa uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya Yanga ikiibuka na ushindi wa mabao 5-0
Dube aliyekuwa aliyeifungia Yanga mabao 13 na kutoa pasi 8 za mabao msimu, alitolewa kunako dakika ya 17 baada ya kupata majeraha ya kuchanika nyama za nyuma ya paja 'hamstring'

Dube huenda akawa nje ya dimba kwa kipindi cha hadi wiki tatu kutibu majeraha hayo na hivyo atakosa mechi zote zilizosalia
Yanga imebakiwa na mechi tatu mbili za ligi kuu na mmoja wa fainali ya kombe la CRDB utakaopigwa visiwani Zanzibaar, Juni 29
Ni wazi Yanga itamkosa Dube katika mchezo dhidi ya Simba utakaopigwa Jumapili, Juni 25 katika uwanja wa Benjamin Mkapa



