CHAN 2025: Sherehe ya Ufunguzi Kifalme Dar es Salaam, Fainali Nairobi

Joel JJ By Joel JJ • 20th June 2025


CHAN 2025: Sherehe ya Ufunguzi Kifalme Dar es Salaam, Fainali Nairobi

Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN 2025) inakaribia kwa kasi, huku maandalizi yakifikia kilele katika nchi tatu zinazoshirikiana kuandaa tukio hili kubwa la soka Tanzania, Kenya, na Uganda.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya CHAN, michuano hii itachezwa katika mfumo wa ushirikiano wa kikanda, hali inayoongeza upekee na uzito wa mashindano haya.

Ufunguzi wa Kihistoria – Agosti 2, Benjamin Mkapa

Tarehe 2 Agosti 2025, macho ya Afrika yote yataelekezwa jijini Dar es Salaam, ambapo sherehe ya uzinduzi wa CHAN 2025 itafanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, moja ya viwanja bora kabisa barani Afrika.

Baada ya sherehe hizo, mchezo wa ufunguzi utapigwa uwanjani hapo, ukiashiria mwanzo rasmi wa safari ya kuelekea ubingwa wa Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani.

Fainali Nairobi, Mechi ya Tatu Kampala

Michuano ya mwaka huu inazidi kuwa ya kipekee kwa sababu fainali itachezwa nchini Kenya katika Uwanja wa Kimataifa wa Kasarani, Nairobi, mnamo Agosti 30, 2025. 

Wakati huo huo, mashabiki wa Uganda pia hawajachwa nyuma, kwani mechi ya kutafuta mshindi wa tatu itafanyika jijini Kampala. Uamuzi huu wa kugawanya mechi muhimu katika nchi tatu za Afrika Mashariki unaashiria umoja, ushirikiano na dhamira ya pamoja ya kukuza soka la Afrika Mashariki

Makundi ya Michuano – Tanzania na Zanzibar Mwenyeji wa Mechi za Makundi

Kundi B: Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam

  • Tanzania

  • Madagascar

  • Afrika ya Kati

  • Burkina Faso

  • Mauritania

Mashabiki wa Tanzania watafurahia kuwaona Taifa Stars wakicheza nyumbani katika uwanja wao wa nyumbani, wakipambana dhidi ya mataifa yenye uzoefu mkubwa katika soka la ndani.

 Kundi D: New Amaan Stadium, Zanzibar

  • Senegal

  • Congo Brazzaville

  • Sudan

  • Nigeria

Kwa upande wa Zanzibar, New Amaan Stadium utakuwa jukwaa la Kundi D, likiwahusisha vigogo wa soka kama Nigeria na Senegal. Hii ni fursa adimu kwa visiwa hivyo kuandaa mechi za kiwango cha juu na kuongeza thamani ya soka la Zanzibar.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.