Local,Normal News,Simba, Yanga

Simba inacheza au haicheza dabi ya Kariakoo?

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jun 2025
Simba inacheza au haicheza dabi ya Kariakoo?

Uongozi wa Simba umeendelea 'kupiga kimya' kuhusu mchezo wa ligi kuu dhidi ya Yanga ambao umepangwa kupigwa Juni 25 2025

Zikiwa zimesalia siku mbili kuelekea mchezo huo, hakuna kiongozi yeyote wa Simba ambaye amekuwa tayari kuzungumzia mchezo huo licha ya Kocha Mkuu Fadlu Davids kuthibitisha kukiandaa kikosi chake kwa ajli ya mchezo huo utakaopigwa Jumatano

Akizungumza baada ya mchezo wa mwisho nyumbani dhidi ya Kagera Sugar ambao Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0, Fadlu alidokeza mabadiliko ya kikosi aliyofanya yalizingatia mkakati wa mechi hiyo ya dabi ya Kariakoo

Hata hivyo Mwenyekiti wa Simba Murtaza Mangungu hakuwa tayari kuzungumzia mchezo huo akisisitiza Simba ni klabu ya mpira wa miguu hivyo kazi yao ni kucheza mpira na hawaihofii timu yoyote

Alipoulizwa Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali alisema jana Simba ilicheza mechi yake ya mwisho katika uwanja wa nyumbani, kama kutakuwa na lolote kuhusiana na mechi hiyo Wanasimba watataarifiwa

"Ratiba inapotoka huhitaji kuthibitisha kama unacheza au la bali unaanza maandalizi kueleke mechi husika. Na mimi nichukue nafasi hii kuwaambia wanasimba taarifa rasmi ni kwamba kama kutakuwa na lolote kuhusiana na mechi ya tarehe 25, tutawaeleza"

"Lakini kwa sasa niseme kwamba tumecheza mchezo wetu wa mwisho nyumbani wa ligi kuu ya NBC 2024/25," alisema Ahmed

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’