Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limemteua Ahmed Arajiga, kuwa mwamuzi wa kati wa mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho (FA) itakayozikutanisha Yanga na Singida Black Stars leo Jumapili.
Arajiga ni mara ya pili mfululizo kuwa mwamuzi wa kati katika fainali ya michuano hii baada ya kuteuliwa msimu uliopita Yanga ilipoifunga Azam kwa penalti 6-5.





