Azam Fc yaanza na Lawi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st July 2025


Azam Fc yaanza na Lawi

Azam Fc imekamilisha usajili wa beki wa Coastal Union na timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Lameck Lawi, imefahamika

Lawi ametua Azam Fc akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba kunako klabu ya Coastal Union

Azam Fc imezipiku klabu za Simba na Yanga katika usajili wa beki huyo mwenye umri wa miaka 20

Msimu uliopita Simba iliingia katika mgogoro na Coastal Union kwa ajili ya beki huyo ambaye hata hivyo mamlaka za soka baadae ziliumuidhinisha kuendelea kuitumikia Coastal Union baada ya Simba kubainika kukiuka makubaliano ya mauziano ya mchezaji huyo

Taarifa za ndani kutoka Azam zinaeleza lengo la kumsajili Lawi ambaye atakwenda kupambania namba na mabeki wa kigeni Yeison Fuentes kutoka Colombia na Yoro Diaby ni kuongeza nguvu kama mzawa.

Kwa beki mzawa anayecheza nafasi hiyo Azam ni Abdallah Kheri aliyekuwa anacheza Pamba kwa mkopo, ambapo uongozi utatathmini alichokifanya kama kinaweza kikaongeza nguvu au la


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.