Azam Fc imekamilisha usajili wa beki wa Coastal Union na timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Lameck Lawi, imefahamika
Lawi ametua Azam Fc akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba kunako klabu ya Coastal Union
Azam Fc imezipiku klabu za Simba na Yanga katika usajili wa beki huyo mwenye umri wa miaka 20
Msimu uliopita Simba iliingia katika mgogoro na Coastal Union kwa ajili ya beki huyo ambaye hata hivyo mamlaka za soka baadae ziliumuidhinisha kuendelea kuitumikia Coastal Union baada ya Simba kubainika kukiuka makubaliano ya mauziano ya mchezaji huyo
Taarifa za ndani kutoka Azam zinaeleza lengo la kumsajili Lawi ambaye atakwenda kupambania namba na mabeki wa kigeni Yeison Fuentes kutoka Colombia na Yoro Diaby ni kuongeza nguvu kama mzawa.
Kwa beki mzawa anayecheza nafasi hiyo Azam ni Abdallah Kheri aliyekuwa anacheza Pamba kwa mkopo, ambapo uongozi utatathmini alichokifanya kama kinaweza kikaongeza nguvu au la



