Local,Transfer News,Simba

Zimbwe Jr kuongeza mkataba mpya Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Jul 2025
Zimbwe Jr kuongeza mkataba mpya Simba

Klabu ya Simba SC ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha dili la kumuongeza mkataba nahodha na beki wa kushoto wa muda mrefu, Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr', ambaye amekuwa nguzo muhimu kwenye kikosi cha wekundu wa Msimbazi kwa misimu kadhaa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba, makubaliano kati ya mchezaji huyo na klabu tayari yamefikiwa, na kilichosalia ni utiaji saini rasmi wa mkataba mpya.

Inaripotiwa kuwa Zimbwe Jr aliomba asaini mkataba mpya baada ya msimu wa 2024/25 kukamilika, jambo ambalo uongozi wa Simba umeliridhia.

Zimbwe Jr, ambaye ni miongoni mwa wachezaji waandamizi na wanaoheshimika ndani ya kikosi hicho, anatarajiwa kuendelea kuitumikia klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili zaidi.

β€œMakubaliano yapo tayari, Zimbwe alionyesha nia ya kubaki na tunathamini mchango wake kwenye timu,” chanzo kutoka ndani ya Simba kilieleza.

Baada ya kukamilika kwa msimu, Simba SC imeanza rasmi mchakato wa kufanya maboresho ya kikosi chake, ambapo hatua ya kwanza ni kuhakikisha wachezaji waliopendekezwa na benchi la ufundi kuendelea wanapewa mikataba mipya kabla ya usajili mpya kuanza.

Zoezi hili ni sehemu ya mpango wa Simba kurejea katika ubora wake, baada ya msimu uliopita kuishuhudia timu hiyo ikikosa mataji ya ndani na pia kukosa taji la Shirikisho (CAF CC)

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’