Local,Normal News,Simba

Simba yajipanga upya kulekea msimu ujao

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Jul 2025
Simba yajipanga upya kulekea msimu ujao

Rais wa heshima na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba Bilionea Mohammed Dewji 'Mo' jana aliongoza kikao cha Bodi kufanya tathmini ya msimu uliopita na kuweka mikakati ya maboresho kuelekea msimu ujao wa mashindano 2025/26

Katika hicho, Bodi ilipata nafasi ya kupitia na kujadili ripoti iliyowasilishwa na Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids ambayo ina mapendekezo yanayohitajika katika kukiboresha kikosi ili kuwa na ushindani zaidi na kushinda mataji msimu ujao

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema kikao hicho ni dalili njema ya mambo mazuri kuelekea maandalizi ya msimu ujao

Ahmed amewataka mashabiki na wanachama wa Simba kuendelea kuwa watulivu wakati mikakati kabambe ikiandaliwa

"Kikao baina ya Bodi ya Wakurugenzi na Baraza la Washauri la klabu yetu ni dalili njema za maandalizi ya msimu ujao. Kwa sasa Wana Simba tuwe watulivu tuwape nafasi viongozi wetu waendeleee na mikakati ya kuitengeneza Simba yetu kwa msimu ujao," alisema Ahmed

Baada ya kikao hicho ni wazi kitakachofuata ni michakato ya maboresho ya kikosi cha Wekundu hao wa Msimbazi kuelekea msimu ujao

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’