Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga Miloud Hamdi amejiunga na klabu ya Ismailia ya ligi kuu ya Misri
Hamdi ametua Ismailia baada ya kumaliza mkataba na klabu ya Yanga
Tetesi za Hamdi kutua Ismailia zilianza kuvuma jana mitandaoni na hatimae yametimia
Yanga sasa inarudi sokoni kusaka Kocha Mkuu atakayechukua mikoba ya Hamdi ambaye pia alichukua mikoba ya Sead Ramovic aliyetimkia CR Belouizdad
Msimu uliomalizika Yanga ilinolewa na makocha watatu ikianza msimu na Miguel Gamondi
Wananchi watamkumbuka Hamdi kwa kuwasaidia kushinda makombe matatu yaani Kombe la Muungano, Ligi Kuu na kombe la CRDB



