Hamdi aitosa Yanga, aibukia Ismaily

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd July 2025


Hamdi aitosa Yanga, aibukia Ismaily

Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga Miloud Hamdi amejiunga na klabu ya Ismailia ya ligi kuu ya Misri

Hamdi ametua Ismailia baada ya kumaliza mkataba na klabu ya Yanga

Tetesi za Hamdi kutua Ismailia zilianza kuvuma jana mitandaoni na hatimae yametimia

Yanga sasa inarudi sokoni kusaka Kocha Mkuu atakayechukua mikoba ya Hamdi ambaye pia alichukua mikoba ya Sead Ramovic aliyetimkia CR Belouizdad

Msimu uliomalizika Yanga ilinolewa na makocha watatu ikianza msimu na Miguel Gamondi

Wananchi watamkumbuka Hamdi kwa kuwasaidia kushinda makombe matatu yaani Kombe la Muungano, Ligi Kuu na kombe la CRDB


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.