Jopo la Mawakili watano kutoka HAKI KWANZA ADVOCATE wamemuwekea pingamizi Rais anaemaliza muda wake Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia kugombea tena nafasi hiyo kwa awamu ya tatu
Mawakili hao wamewasilisha pingamizi Baraza la Michezo la Taifa (BMT) wakipinga kitendo cha Karia kuchukua 'endorsement' 46 kati ya 47. Endorsement moja ambayo haijamilikiwa ni ya klabu ya Yanga
Jopo hilo la Mawakili pia linapinga kuhusu ukiukwaji wa sera ya michezo inayoeleza ukomo wa viongozi madarakani
Kwa mujibu wa sera hiyo, nafasi za uongozi wa miaka minne ukomo wake ni vipindi viwili na uongozi wa miaka mitatu ukomo wake ni vipindi vitatu
Karia tayari ameiongoza TFF vipindi viwili vya miaka minne minne na hivyo Mawakili hao wanaamini kama ataruhusiwa kugombea tena itakuwa kinyume na sera hiyo



