Karia awekewa pingamizi BMT

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd July 2025


Karia awekewa pingamizi BMT

Jopo la Mawakili watano kutoka HAKI KWANZA ADVOCATE wamemuwekea pingamizi Rais anaemaliza muda wake Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia kugombea tena nafasi hiyo kwa awamu ya tatu

Mawakili hao wamewasilisha pingamizi Baraza la Michezo la Taifa (BMT) wakipinga kitendo cha Karia kuchukua 'endorsement' 46 kati ya 47. Endorsement moja ambayo haijamilikiwa ni ya klabu ya Yanga

Jopo hilo la Mawakili pia linapinga kuhusu ukiukwaji wa sera ya michezo inayoeleza ukomo wa viongozi madarakani

Kwa mujibu wa sera hiyo, nafasi za uongozi wa miaka minne ukomo wake ni vipindi viwili na uongozi wa miaka mitatu ukomo wake ni vipindi vitatu

Karia tayari ameiongoza TFF vipindi viwili vya miaka minne minne na hivyo Mawakili hao wanaamini kama ataruhusiwa kugombea tena itakuwa kinyume na sera hiyo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.