Newcastle imewasilisha ofa iliyoboreshwa ya pauni milioni 55 kwa winga wa Uswidi Anthony Elanga, 23, na iko mbioni kukubaliana na Nottingham Forest. (Mail)
Real Madrid na kocha Xabi Alonso wamefikia makubaliano ya kuuzwa kwa mshambuliaji wa Brazil Rodrygo, ambaye amekuwa akihusishwa na Arsenal, ikiwa ofa stahiki itatolewa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Athletic - usajili unahitajika)
Fenerbahce imewasilisha ofa ya euro milioni 15 (£12.9m) kwa mshambuliaji wa Paris St-Germain Marco Asensio lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 anasubiri chaguzi nyingine kutokea, huku klabu za AC Milan na Villarreal zikimtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania. (L'Equipe - kwa Kifaransa)
Como wamekubali ofa ya awali ya £16.5m kwa winga wa Celtic Mjerumani Nicolas Kuhn, 25. (Sky Sports)
Rangers iko mbioni kukamilisha dili la kiungo wa Luton Town na Norway Thelo Aasgaard, 23. (Daily Record)
Tottenham Hotspur na Chelsea ni miongoni mwa klabu zinazomwinda kiungo wa AZ Alkmaar Mholanzi Kees Smit, 19. (TBR Football)
Al-Nassr huenda ikaelekeza darubini yake kwa winga wa Arsenal Mbrazili Gabriel Martinelli, 24, baada ya kushindwa kumsajili - mshambuliaji wa Liverpool na Colombia Luis Diaz, 28 amabye alikuwa lengo lao kuu. (GiveMesport)
Beki wa Inter Milan na Uholanzi Denzel Dumfries, 29, ana kipengele cha kutolewa cha euro 25m (£21.5m) katika kandarasi yake ambayo itatumika hadi katikati ya Julai na inaweza tu kuzingatiwa na klabu isiyo ya Italia. (Calciomercato - kwa Kiitaliano)
Mchezaji wa kimataifa wa Ureno Antonio Silva, 21, amekataa ombi la kuhamia klabu ya Al-Hilal ya Saudia, lakini beki huyo wa kati bado anatarajiwa kuondoka Benfica. (A Bola - kwa Kireno) Arsenal wamempoteza meneja wao wa chini ya miaka 21 Mehmet Ali aliyeamua kujiunga na Brentford. (Football London)
BBC



