Kagera Sugar yaachana na CEO

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th July 2025


Kagera Sugar yaachana na CEO

Klabu ya Kagera Sugar imetangaza kutokumuongezea mkataba aliyekuwa Mtendaji Mkuu Thabit Kandoro

Taarifa iliyotolewa na Kagera Sugar, imemtakia kila la kheri Kandoro ambaye anaondoka baada ya timu hiyo kushuka daraja

"Uongozi wa Kagera Sugar Football Club unapenda kuutarifu Umma, mashabiki wetu, wanamichezo, na wadau wote wa michezo kuwa klabu imefikia makubaliano rasmi ya kutomuongeza mkataba mpya Mtendaji Mkuu wa Klabu THABITY KANDORO baada ya mkataba wake wa awali kufikia ukomo mwishoni mwa msimu huu wa NBCPL 2024/2025.

Uamuzi huu umefikiwa kwa maelewano na heshima kubwa kati ya pande zote mbili, huku klabu ikimshukuru sana kwa mchango wake mkubwa katika kipindi chote alichoitumikia klabu.

Uongozi unamtakia kila la heri katika majukumu yake mapya ya baadae. Tunaahidi kuendelea kuimarisha mifumo ya kiutendaji ndani ya klabu na tutatoa taarifa rasmi kuhusu mchakato wa kumpata mrithi wake katika muda muafaka.

Tunawaomba mashabiki wetu waendelee kutuunga mkono Katika kipindi hiki ambacho tunafanya maboresho ya kikosi pamoja na Benchi la ufundi kuelekea msimu mpya wa NBC CHAMPIONSHIP 2025/2026."


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.