Kuelekea msimu mpya wa michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na kombe la Shirikisho, Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) tayari limetangaza rasmi kuwa mashindano hayo kwa msimu wa 2025/26 yataanza mwezi Septemba.
Mabadiliko haya ya ratiba yamesababishwa na kuandaliwa kwa mashindano ya CHAN yatakayofanyika mwezi Agosti nchi za Kenya, Uganda na Tanzania





