Kuelekea msimu mpya wa michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika na kombe la Shirikisho, Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) tayari limetangaza rasmi kuwa mashindano hayo kwa msimu wa 2025/26 yataanza mwezi Septemba.
Mabadiliko haya ya ratiba yamesababishwa na kuandaliwa kwa mashindano ya CHAN yatakayofanyika mwezi Agosti nchi za Kenya, Uganda na Tanzania
Yanga wakiwa mabingwa wa ligi kuu ya NBC wataiwakilisha Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa sambamba na Simba iliyomaliza katika nafasi ya pili wakati Azam Fc na Singida BS wakishiriki kombe la Shirikisho
Habari njema kwa klabu ya Simba ni kuwa haitashiriki raundi ya kwanza ya michuano hiyo ikiwa miongoni mwa vigogo watano Afrika waliokusanya alama nyingi katika kpindi cha miaka mitano
Hatua ya Awali ya Kwanza:
Mchezo wa kwanza: Septemba 19β21, 2025
Mchezo wa marudiano: Septemba 26β28, 2025
Hatua ya Awali ya Pili:
Mchezo wa kwanza: Oktoba 17β19, 2025
Mchezo wa marudiano: Oktoba 24β26, 2025
Mechi za Maundi:
Siku ya mechi 1: Novemba 21β23, 2025
Siku ya mechi 2: Novemba 28β30, 2025
Siku ya mechi 3: Januari 23β25, 2026
Siku ya mechi 4: Januari 30βFebruari 1, 2026
Siku ya mechi 5: Februari 6β8, 2026
Siku ya mechi 6: Februari 13β15, 2026
Hatua ya Mtoano (Knockout):
Robo Fainali:
Mchezo wa kwanza: Machi 13β15, 2026
Mchezo wa marudiano: Machi 20β22, 2026
Nusu Fainali:
Mchezo wa kwanza: Aprili 10β12, 2026
Mchezo wa marudiano: Aprili 17β19, 2026
Fainali:
Imepangwa kuchezwa kati ya Mei 8 na 24, 2026
Vipindi vya Usajili wa Wachezaji:
CAF pia imethibitisha dirisha la usajili kwa vilabu vitakavyoshiriki:
Usajili wa Hatua ya Awali: Agosti 1β31, 2025
Usajili wa Hatua ya Awali ya Pili: Septemba 1β30, 2025
Usajili wa Hatua ya Makundi: Oktoba 1β31, 2025
Usajili wa Hatua ya Mtoano: Januari 1β31, 2026



