International,Transfer News

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne Julai 08 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Jul 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne Julai 08 2025

Tottenham, Newcastle na Napoli zote zinamfuatilia kiungo wa England Jack Grealish baada ya Manchester City kuweka bei ya pauni milioni 40 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 (Sun).

Newcastle United wanaendelea kuwa na matumaini ya kushinda mbio za kumsajili Marc Guehi, 24, huku klabu hiyo ikitaka kuimarisha kikosi chao kwa kumuongeza beki wa kati huyo wa England na Crystal Palace (GiveMeSport).

Crystal Palace wenyewe wako kwenye mazungumzo na Sporting kuhusu uwezekano wa mpango wao wa pauni milioni 45 kumnasa beki wa Ivory Coast Ousmane Diomande, 21 (Guardian).

Newcastle pia wamefanya mazungumzo mapya na Dominic Calvert-Lewin, 28, huku meneja Eddie Howe akiwa shabiki wa muda mrefu wa mshambuliaji huyo wa England aliyeondoka Everton baada ya mkataba wake kumalizika mwezi uliopita. Anasakwa pia na maslahi kutoka Manchester United (Talksport).

Beki wa West Ham mwenye umri wa miaka 29 kutoka Morocco, Nayef Aguerd, anasakwa kwa udi na uvumba na klabu ya Ufaransa Marseille msimu huu wa joto (L'Equipe).

Manchester United wamefanya jaribio la kumsajili kiungo wa Atalanta na Brazil Ederson, huku vilabu viwili vya Serie A Inter Milan na Juventus pia vikimfuatilia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 mwenye thamani ya takriban pauni milioni 44 (Goal).

Mshambuliaji wa Denmark Rasmus Hojlund, 22, hafikirii kuondoka Manchester United isipokuwa kama klabu itaamua kumuuza, huku Inter Milan ikiwa moja ya vilabu vilivyoonyesha nia ya kumsajili (Fabrizio Romano).

Wakati huo huo, Manchester United waliweka ada ya uhamisho ya pauni milioni 30 kwa Andre Onana kwa AS Monaco mwishoni mwa mwezi uliopita, lakini kipa huyo wa Cameroon mwenye umri wa miaka 29 anaonekana kwa asilimia kubwa atabaki klabuni (Mail).

Manchester United pia wanavutiwa na kiungo wa Nigeria Wilfred Ndidi, 28, ambaye anaripotiwa kuwa katika mkataba wake kuna kipengele cha kuuzwa kwa pauni milioni 9 kutokana na kushuka daraja kwa Leicester City, huku Fulham, Everton na Crystal Palace pia wakimwania (Tuttosport).

Beki wa Italia Davide Calabria, 28, pia anasakwa na Crystal Palace. Alikuwa kwenye kiwango bora akiwa kwa mkopo Bologna msimu uliopita lakini sasa ni mchezaji huru baada ya kuondoka AC Milan mkataba wake ulipoisha (Sky Sports).

Sunderland, Leeds United na Wolves wanavutiwa na kiungo wa Lens na timu ya Morocco Under-23 Neil El Aynaoui, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka AS Roma, Juventus na AC Milan kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 (Footmercato).

Meneja wa Slavia Prague Jindrich Trpisovsky amethibitisha kuwa El Hadji Malick Diouf yuko tayari kuondoka klabuni huku West Ham na Leeds zikihusishwa na beki huyo wa Senegal mwenye umri wa miaka 20 (Standard).

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
47m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’