Klabu ya Fountain Gate FC imefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya kupata ushindi wa jumla wa mabao 5-1 dhidi ya Stand United katika michezo miwili ya mtoano (play-off).
Katika mchezo wa marudiano uliochezwa kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara, Fountain Gate ilionyesha dhamira ya kusalia ligi kuu kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.





