Kiungo Clatous Chama raia wa Zambia, yuko mbioni kujiunga na klabu ya Azam Fc, imefahamika
Chama alikuwa katika mazungumzo ya kuongeza mkataba na Yanga lakini inaelezwa mazungumzo hayo yemevunjika
Mkataba wake umemalizika, ni mchezaji huru, taarifa ya duru za usajili imethibitisha Chama kufanya mazungumzo na Azam Fc ambayo yamefikia mwafaka na nyota huyo huenda akaelekea Chamazi
Baada ya kupata mafanikio makubwa na klabu ya Simba, Chama amedumu Jangwani kwa msimu mmoja tu akifunga mabao sita na kutoa pasi nne za mabao katika ligi kuu
Chama anakwenda kuingia katika orodha ya wachezaji waliozitumikia timu kubwa tatu nchini yaani Yanga, Simba na Azam Fc



