Azam Fc na Chama ni suala la muda

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th July 2025


Azam Fc na Chama ni suala la muda

Kiungo Clatous Chama raia wa Zambia, yuko mbioni kujiunga na klabu ya Azam Fc, imefahamika

Chama alikuwa katika mazungumzo ya kuongeza mkataba na Yanga lakini inaelezwa mazungumzo hayo yemevunjika

Mkataba wake umemalizika, ni mchezaji huru, taarifa ya duru za usajili imethibitisha Chama kufanya mazungumzo na Azam Fc ambayo yamefikia mwafaka na nyota huyo huenda akaelekea Chamazi

Baada ya kupata mafanikio makubwa na klabu ya Simba, Chama amedumu Jangwani kwa msimu mmoja tu akifunga mabao sita na kutoa pasi nne za mabao katika ligi kuu

Chama anakwenda kuingia katika orodha ya wachezaji waliozitumikia timu kubwa tatu nchini yaani Yanga, Simba na Azam Fc


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.