Beki wa kati wa Simba Che Malone Fondoh anahusishwa na klabu ya USM Alger ya Algeria, imefahamika
Kwa mujibu wa mwanahabari maarufu wa Ghana Micky Junior, mazungumzo baina ya Che Malone na klabu hiyo yanaendelea
Che Malone amemaliza mkataba na Simba, mpaka sasa hakuna uhakika kama ataendelea kusalia Msimbazi msimu ujao
Aidha inaelezwa Simba iko kwenye mazungumzo na beki raia wa Ivory Coast Souleymane Coulibaly ambaye msimu uliopita aliitumikia Asec Mimosas

Coulibaly tayari yuko jijini Dar es salaam kukamilisha taratibu za usajili kujiunga na Wekundu hao wa Msimbazi
Kama Simba itakamilisha usajili huo ni wazi mpango wa kumbakisha Che Malone utafutika



