USM Alger yapiga hodi Msimbazi kumtaka Che Malone

Joel JJ By Joel JJ • 11th July 2025


USM Alger yapiga hodi Msimbazi kumtaka Che Malone

Beki wa kati wa Simba Che Malone Fondoh anahusishwa na klabu ya USM Alger ya Algeria, imefahamika

Kwa mujibu wa mwanahabari maarufu wa Ghana Micky Junior, mazungumzo baina ya Che Malone na klabu hiyo yanaendelea

Che Malone amemaliza mkataba na Simba, mpaka sasa hakuna uhakika kama ataendelea kusalia Msimbazi msimu ujao

Aidha inaelezwa Simba iko kwenye mazungumzo na beki raia wa Ivory Coast Souleymane Coulibaly ambaye msimu uliopita aliitumikia Asec Mimosas

 Coulibaly tayari yuko jijini Dar es salaam kukamilisha taratibu za usajili kujiunga na Wekundu hao wa Msimbazi

Kama Simba itakamilisha usajili huo ni wazi mpango wa kumbakisha Che Malone utafutika


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.