Klabu ya Simba inatajwa kuwa katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wa beki wa kati wa JKT Tanzania n timu ya Taifa, Wilson Nangu
Nangu mwenye umri wa miaka 23 anatua Msimbazi akiwa ni pendekezo la Kocha Fadlu Davids akichukua nafasi ya Hussein Kazi ambaye tayari Simba imethibitisha kuachana nae baada ya mkataba wake kumalizika
Licha ya kumudu kucheza kama beki wa kati, Nangu pia anaweza kutumika katika nafasi zote za ulinzi wa pembeni yaani kulia na kushoto
Hivyo ni beki kiraka ambaye anawez kutumika popote katika safu ya ulinzi ingawa eneo analomudu zaidi ni beki wa kati
Pamoja na kumnasa Nangu, Simba pia huenda ikamn'goa mlinda lango wa JKT Tanzania Yacoub Mohammed



