Local,Transfer News,Yanga

Dili la Mzize kutua Zamalek utata

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Jul 2025
Dili la Mzize kutua Zamalek utata

Mshambuliaji wa Yanga SC, Clement Mzize, bado yuko njia panda kuhusu hatma yake ya kutua klabu ya Zamalek ya Misri, licha ya awali kuonekana kama dili lililokamilika.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya karibu na mchezaji huyo, tayari Yanga ilikuwa imekubaliana na Zamalek kuhusu uhamisho wake, lakini mvutano wa kimaslahi kati ya wasimamizi wa Mzize na klabu hiyo ya Cairo umechelewesha dili hilo.

Mzize, ambaye msimu uliopita aliibuka kuwa mmoja wa wafungaji bora katika Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kufunga mabao 14, yakiwa mawili nyuma ya kinara Jean Charles Ahoua wa Simba SC, ameendelea kuvutia vilabu vya nje, ikiwemo Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.

Hata hivyo, tetesi za uhamisho wake Kaizer Chiefs zinaonekana kufifia, hasa baada ya klabu hiyo kuanza rasmi maandalizi ya msimu mpya (pre-season) bila uwepo wa mshambuliaji huyo.

Iwapo sintofahamu kati ya wasimamizi wa Mzize na Zamalek haitatatuliwa hivi karibuni, kuna kila dalili kuwa mshambuliaji huyo atasalia Jangwani kwa msimu mwingine akiwa bado na mkataba wa miaka miwili na Yanga

Mzize yuko na kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kilichoweka kambi Misri kujiandaa na michuano ya CHAN inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za ndani inayoanza August 02 na kufikia tamati August 30

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’