Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne, Julai 15 2025

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th July 2025


Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne, Julai 15 2025

Arsenal inajiandaa kuwasiliana na Crystal Palace kujadili iwapo inaweza kumsajili winga wa Uingereza Eberechi Eze bila kuanzisha kipengele cha kutolewa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kwa pauni milioni 68. (Sportsport)

Liverpool imefanya mazungumzo na mshambuliaji wa Crystal Palace Jean-Philippe Mateta, 28. Mfaransa huyo amekutana na wawakilishi wa klabu hiyo mjini Paris. (Footmercato - kwa Kifaransa)

Manchester United imefikia makubaliano na Brentford kumsajili mshambuliaji wa Cameroon Bryan Mbeumo, 25. (UFootball Transfers)

Brentford inafikiria kumsajili winga wa Ipswich Town na England aliye na umri wa miaka 21 Omari Hutchinson kama mbadala wa Mbuemo. (Standard)

Wakala wa Joao Felix amekuwa akisaidia katika mazungumzo ya mshambulizi wa Chelsea mwenye umri wa miaka 25 kuhamia Benfica. (A Bola - kwa Kireno)

Chelsea inavutiwa sana na winga wa Manchester United na Argentina Alejandro Garnacho, 21, baada ya kufanya mazungumzo ya awali mwezi Januari, (TBR Football)

West Ham imewaongeza wachezaji wawili wa Liverpool walio chini ya umri wa miaka 21, mshambuliaji Harvey Elliott, 22, na kiungo mkabaji Tyler Morton, 22, kwenye orodha ya walengwa. (Mail)

Manchester United imewasiliana na klabu ya Lyon kuhusu kiungo wa kati wa Ufaransa Corentin Tolisso, 30. (L'Equipe - kwa Kifaransa)

Mshambuliaji wa kimataifa wa Gabon na mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Pierre-Emerick Aubameyang, 36, anatarajiwa kuondoka Al-Qadsiah ya Saudi Arabia na kujiunga na klabu ya Ufaransa ya Marseille. (La Provence - kwa Kifaransa)

Manchester City itamuuza kiungo wa kati wa England chini ya umri wa miaka 21 James McAtee, 22, msimu huu wa kiangazi kwa lengo la kunufaika kutokana na Kanuni za Faida na Uendelevu (PSR) na sheria zinazodhibiti matumizi ya klabu (FFP). (Football Insider)

McAtee yuko nchini Ujerumani kutembelea Eintracht Frankfurt kama sehemu ya mpango wa klabu amabayo huenda akajiunga nayo. (Fabrizio Romano)

Wolves inakaribia kufikia mkataba wa pauni milioni 15 kwa winga wa Fluminense na Colombia Jhon Arias, 27. (Mail)

Kiungo wa kati wa Uswizi Granit Xhaka amekubali kujiunga na klabu ya Saudi Pro Neom SC, ambayo bado haijakamilisha ada na Bayer Leverkusen kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32. (Sky Sports Ujerumani)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.